Saturday, July 27, 2024

Jifunze, Chukua Hatua Kuboresha Afya Yako

Afya ya uzazi

WANAWAKE KULAMBWA UKE HUWEZA KUSABISHA MAGONJWA YA UKE, KIZAZI NA UGUMBA.TAFITI

Jarida moja nchini marekani kwa jina la PLOS limechapisha tafiti mpya ambayo inasema kwamba tabia ya kulamba uke wakati wa tendo la ndoa linachangia sana wanawake kupata maambukizi ya fangasi na magonjwa mengine ya uke mara kwa mara hali ambayo huweza kusababisha usugu na kushindwa kutibika kabisa..Dalili za magonjwa haya ni kama kuwashwa, kutoka uchafu na harufu kali kutoka ukeni.

Ugonjwa wa uke kitaalamu kama vaginosis huweza kupanda mpaka kwenye kizazi na kusababisha magonjwa ya kizazi kama PID ambayo hupelekea ugumba mara nyingi.

Chanzo ni nini?

Kiasilia uke una aina fulani ya bacteria ambao huulinda ili usiweze kuambukizwa magonjwa mbalimbali lakini pia kuna hali ya tindikali au acid ambayo pia ni kama njia ya ulinzi wa uke, sasa uke unavyonyonywa au kulambwa kuna bacteria wengi wa mdomoni ambao wakiwa mdomoni hawana shida lakini wakifika kwenye uke husababishwa magonjwa.

Bacteria wa fusobacterium ambao hupatikana kwenye mate mdomoni ni moja ya bacteria ambao wameonekana kuhusika sana na magonjwa ya uke lakini pia ulambaji wa uke hupunguza kiasi cha tindikali ambacho kinalinda uke na kusababisha magonjwa ya kuwashwa mara kwa mara ambayo ndio fangasi.

Tafiti hizi zinakuja baada ya tafiti za mwanzo ambazo zilionyesha kwamba walambaji wa sehemu za siri yaani uke au uume wana hatari ya kuugua saratani ya koo ambayo hupatikana kwa kulamba virusi vya HPV ambavyo hupatikana sehemu hizo.

Virusi vya HPV husabisha saratani ya shingo ya uzazi lakini vikilambwa na kwenda kwenye koo husababisha saratani ya koo.

Ushauri; Wataalamu wanashauri kutolamba sehemu za siri za mtu yeyote hata kama ni mke wako au mme wako kwani tafiti zinaonyesha kuongezeka kwa magonjwa ambayo yanatokana na tabia hizo.

STAY ALIVE

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *