Saturday, July 27, 2024

Jifunze, Chukua Hatua Kuboresha Afya Yako

Afya ya uzazi

TATIZO LA WATOTO WACHANGA KUINGIA HEDHI NA MATIBABU YAKE (FALSE MENSES)

Moja ya vitu vya kuogopa na kushtukiza kwa wamama ni kutoka kwa damu ya hedhi kwa mtoto mchanga ambaye ayezaliwa ndani ya kama siku mbili mpaka kumi hapo, na anaweza kukimbia hospitali haraka huku amechanganyikiwa.

chanzo ni nini?

Mama akiwa mjamzito homoni za uzazi yaani oestrogen na progesterone zinakua juu sana kiasi kwamba wakati mwingine zinakua zinamuathiri mpaka mtoto, moja ya kazi ya homoni ya oestrogeni ni kujenga ukuta wa seli ndani ya kizazi kitaalamu kama endometrial hyperplasia. Baada ya kujifungua homoni zile hushuka ghafla kwenye mwili wa mtoto na kufanya ukuta ule kushindwa kustahimili hivyo kuanguka kwa kutoa damu ambayo hutoka kama hedhi. Asilimia tano ya watoto wanaozaliwa hupata hali hii.

Nini cha kufanya?

Damu ili haitatoka kwa siku kadhaa kama hedhi zingine lakini itatoka tu ndani ya muda mfupi cha msingi endelea kumkagua na kumfanyia usafi na mara nyingi damu hiyo huisha yenyewe. Kama damu zikiendelea kutoka nyingi au kuanza kutoa harufu basi mpeleke mtoto hospitali.

STAY ALIVE

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *