FAHAMU JINSI YA KUTAMBUA DALILI ZA MWANZO ZA MTOTO MGONJWA KABLA HAJAZIDIWA ZAIDI.
Watoto wadogo hasa chini ya mwaka mmoja au miwili hawana uwezo wa kuongea hivyo wakianza kuugua unaweza usijue mpaka mtoto azidiwe kabisa ndio unaanza kukimbia usiku kutafuta msaada, sasa watoto wale ni rahisi sana kufariki kuliko watu wazima hivyo kugundua dalili za ugonjwa mapema ni vizuri zaidi kuliko kusubiri dalili za wazi..
Wazazi wengi hasa wazazi wapya wanakua wanafahamu kwamba dalili za kuugua mtoto zinakua wazi kama za watu wote kwa maana nyingine husubiri mpaka mtoto atapike, aharishe,ashindwe kupumua au apate degedege ndio ujue anaumwa.
Kuna dalili za mwanzo kabisa ambazo ukiziona ni vizuri kwenda hospital mapema, hii itamfanya mtoto atibiwe mapema na kuepusha adha zingine kama kulazwa, kutumia gharama kubwa za matibabu, kuugua sana na kupata madhara au kifo.
Mtoto wa kawaida hua na hamu nzuri ya kula, analala vya kutosha, anakua na nguvu na anakua mtundu na mchunguzi sana kwenye mazingira yanayomzunguka.
dalili za kwanza za mtoto mgonjwa ni kama ifuatavyo…….
kulia sana hata akiguswa kidogo tu.
kuacha kucheza.
kua mkimya sana.
kuonekana mchovu sana
kukataa kula
joto la mwili kuanza kubadilika.
Mara nyingi hizi ni dalili za mwanzo kabisa na ukizipuuzia mtoto huingia kweye hatua ya pili ambayo huzidiwa sana na kuhatarisha maisha yake hivyo ni vizuri kuwahi hospital.
usitoe dawa yeyote kwa mtoto mgonjwa hata kama ni panado, hiyo sio dawa ya kutibu na huweza kuficha dalili za ugonjwa halisi na kumpa shida daktari.
STAY ALIVE
Thanks for sharing. I read many of your blog posts, cool, your blog is very good.
Your article helped me a lot, is there any more related content? Thanks!
Thank you for your sharing. I am worried that I lack creative ideas. It is your article that makes me full of hope. Thank you. But, I have a question, can you help me?
Thank you for your sharing. I am worried that I lack creative ideas. It is your article that makes me full of hope. Thank you. But, I have a question, can you help me?
Can you be more specific about the content of your article? After reading it, I still have some doubts. Hope you can help me.
Hey there! Would you mind if I share your blog with my facebook group? There’s a lot of people that I think would really appreciate your content. Please let me know. Thank you